Facebook

Monday, 2 June 2014

Diamond aweka historia New Jersey

 All Star Club Elizabeth New Jersey Diamond akikamua licha ya show kuchelewa kuanza na wapenzi wa Diamond kushikwa na jazba wakitaka aendelee lakini ikashindika kutokana na muda wa kufunga club kufika.
 AJ nae akifanya yake baada ya kupewa nafasi ya ufunguzi katika show hiyo iliyofanyika New Jersey.
AJ Ubao na Dirty Hary wakishambulia jukwaa kwenye show ya kufungua pazia iliyoanyika New Jersey na baadae Prezidaa wa Wasafi, Diamond Plutnumz kuwapagawisha mashabiki wake wa ukanda wa pwani ya mashariki.
Ni Rais wa Wasafi akishambulia jukwaa akiwa na madancer wake kwenye show ya kukata na shoka iliyofanyika New Jersey na kuvuta mashabiki kutoka kila kona ya pwani ya mashariki ambayo ni DC, PA, NJ, NY, CT, MA na kwingineko
Diamond mwanamuziki wa kizazi kipya anayekimbiza vibaya mno kwenye anga za Bongo Flava akipagawisha mashabiki wake New Jersey nchini Marekani.
Diamond na madancer wake wakijaribu kukata kiu ya mashabiki wake wa pwani ya mashariki.
 Wapenzi wa Diamond wakipagawa na show ya Diamond iliyofanyika All Star Club Elezabeth NJ.


Shabiki akidata na show ya prezidaa wa wasafi.

Shabiki akidatishwa na moja ya wimbo wa Diamond na kushindwa kujizuia kupanda jukwaani.

Mashabiki wa Diamond wakipagawa huku wengine wakipata taswira za hapa na pale.

Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata habari mbalimbali kwa wakati na muda muafaka

Related Posts:

  • Birthday ya Vicenti Kigosi "ray", Johari ampa salamu tata !! Jana mwigizaji maarufu nchini Vicent kigosi - Ray amesherehekea siku yake ya kuzaliwa huku akipata salamu mbalimbali za pongezi toka kwa mastaa mbalimbali nchini. Moja ya watu wa kwanza kw… Read More
  • Wema mama Kijacho,anasa mimba ya Diamond.! ‘Beautiful  Onyinye’  na  kipenzi  cha  Diamond, Wema  Sepetu  sasa  ni  mjamzito. Baada  ya  misukosuko  ya  muda  mrefu  ikiwemo  kuporwa … Read More
  • Penny afunguka baada ya kupona. MTANGAZAJI wa maarufu wa runinga Bongo, Peniel Mungilwa ‘Penny’ amefunguka kuwa ugonjwa uliompiga juzikati ulikuwa ‘serious’ kiasi cha kuona ni Mungu tu amemwokoa. Akichezesha taya na paparazi wetu, Penny al… Read More
  • Rapper Eve aolewa   Msanii maarufu wa miondoko ya kufokafoka - rap- nchini Marekani Eve, ameoana rasmi na mchumba wake Maximillion Cooper, katika mji wa Ibiza nchini Spain. Cooper ni muasisi wa mashindano ya mbio za magari za Gumb… Read More
  • Alichokisema Wema Sepetu Kuhusu Penzi lake na Diamond. Wema Sepetu amesema uhusiano wake na Diamond Platnumz kwa sasa ni imara kwa kuwa wamepitia mambo mengi pamoja yaliyowafunza mengi. Akiongea hivi karibuni akiwa jijini Durban, Afrika Kusini alikoenda kuhudhuria t… Read More

0 comments:

Post a Comment