Facebook

Tuesday, 3 June 2014

Urusi yapiga marufuku uvutaji wa sigara kwenye masoko, migahawa na mahotelini

sigara1
Ile sheria ya kupambana na uvutaji sigara imeanza kutumika nchini Urusi ambapo sasa ni marufuku kuvuta sigara katika migahawa na maeneo mengine ya kupata huduma za chakula.
Marufuku hiyo pia inatumika katika mahoteli na masoko ikiwa ni pamoja na kwenye vyombo vya usafiri kama treni na meli na katika vituo vya treni za masafa marefu.
Курение в общественных местах
Wamiliki wa migahawa na sehemu nyingine za kula wanatakiwa kuondoa vyombo vya kuwekea majivu ya sigara na kubandika matangazo ya onyo la kuvuta sigara kuwatahadharisha wateja kuwa uvutaji wa sigara ni marufuku katika maeneo hayo.
Mmiliki wa kawaida wa maeneo hayo atalazimika kulipa faini ya dola za kimarekani 870 hadi 1150 ikiwa mmoja wa wateja wake atakutwa akivuta sigara. Hii ni pamoja na wamiliki wa biashara kubwa ambao watalipa hela nyingi zaidi kiasi cha dola 1,700 hadi 2,600 kwa kosa kama hilo.
Мужчина держит в руках сигарету
Asilimia 82 ya wamiliki wa migahawa nchini Urusi wanaamini marufuku hiyo ya uvutaji sigara ni unyanyasaji wa moja kwa moja kwa wavutaji na kutarajia idadi kubwa ya wageni kuanzia siku ya kuanza kutumika kwake.



Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari,tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi hivi karibuni.

Related Posts:

  • Kijana wa miaka 17 apunguzwa uume Mvulana mmoja amefanyiwa kile madaktari wanasema ni upasuaji wa kwanza wa kupunguza uume wake. Kijana huyo wa miaka 17 alikuwa akilalamika kwamba hangeweza kushiriki katika tendo la ngono ama hata kushiriki katika michezo… Read More
  • Haya ndiyo yanayoweza kufanyika iwapo mtumiaji wa Facebook amefariki. Mitandao ya kijamii imetusogeza karibu, Facebook ni moja ya mitandao hiyo, lakini kurasa za mtumiaji wa mtandao kama Facebook huwa zinaendelea kuwepo hata kama ikitokea mtumiaji amefariki. Facebook wameenda mb… Read More
  • Mbwa kitoweo murua China,Wawashangaa WaTanzania. Baadhi ya wachina waishio Tanzania hapo jana waliungana na wenzao duniani kuadhimisha mwaka mpya wa kichina. Hata hivyo wakati wachina hao wakiadhimisha mwaka huo baadhi ya raia wa Tanzania wamekuwa wakistaajabu vy… Read More
  • Msikiti mkubwa Afrika wajengwa Algeria Msikiti utakaoshindana na maeneo mengine ya Kiislam ya kuabudia makubwa kuliko yote duniani unajengwa katika pwani ya kaskazini mwa Algeria. Nini malengo ya kujenga msikiti mkubwa kama huu? Nusu ya eneo katika ghuba ya Al… Read More
  • Wezi wa kompyuta waiba dola bilioni 1 Genge la wezi wa kompyuta limefanikiwa kuiba takriban dola bilioni moja kutoka kwenye akaunti za wateja wa mabenki 100 katika mataifa 30. Kampuni inayosimamia usalama wa programu ya kompyuta inayohakikisha data ya wate… Read More

0 comments:

Post a Comment