Facebook

Saturday, 7 June 2014

Bin Slum Tyres Company Limited yaingia mkataba wa miaka miwili na Mbeya City


Kampuni ya Binslum Tyres Co. Ltd....chini ya Mkurugenzi wake, Nassor Binslum sasa imeingia mkataba wa miaka miwili wa shilingi 360 milioni na klabu ya Mbeya City ya jijini Mbeya.
 
 
Katika mwaka wa kwanza, Mbeya City itapokea kiasi cha shilingi 180 milioni, na mwaka wa pili itapokea kiasi kama hicho....watavaa jezi yenye nembo ya RB ikiwa ni betri maarufu za kampuni hiyo. 

Kampuni ya Bin Slum Tyre Company Limited leo imeingia mkataba rasmi wa kuidhamini timu ya soka ya Mbeya City Council ya jijini Mbeya katika hafla fupi ya utiaji saini mkataba huo uliyofanyika katika ukumbi wa ofisi za jiji la Mbeya.
Mkataba huu utakuwa wa miaka miwili, ambao utawafanya Mbeya City kunufaika na kiasi hicho cha fedha kwa muda huo wote wa mkataba.
Akiongea wakati wa utiaji saini wa mkataba huo jijini Mbeya, Mkurugenzi wa , Binslum Tyre Mohamed Binslum, alisema “Tumefikia makubaliano haya baada ya kuona uongozi wa timu ya Mbeya City umejipanga vizuri katika kuendesha timu yao, na kupata mwitikio mkubwa kutoka kwa wananchi wa Jiji la Mbeya pamoja na mikoa ya Kanda ya Kusini, hivyo itakuwa ni fursa nzuri kwa kuzitangaza betri zetu za RB ambazo pia Mbeya ni soko letu kubwa”.” Kampuni yetu ina bidhaa nyingi kama vile aina nzuri ya matairi ya Double Star na Vee Rubber”. Aliongeza Binslum



Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari,tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.

Related Posts:

  • MATOKEO YAZUA VURUGU ARGENTINA   Polisi wa Argentina wamepambana na waandamanaji katika mji mkuu, Buenos Aires baada ya nchi hiyo kufungwa na Ujerumani katika mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia. Mapema jana jioni maelfu ya watu walikusanyika… Read More
  • ADHABU YA POWELL YAPUNGUZWA    Bingwa wa zamani wa mbio za mita 100 Asafa Powell na Sherone Simpson wote kutoka Jamaica wamepunguziwa adhabu ya kufungiwa, kutoka miezi 18 hadi miezi sita. Uamuzi uliotolewa na mahakama ya usuluhisi wa m… Read More
  • Ujeruman yapokelewa kwa shangwe.   Maelfu ya mashabiki wa soka nchini Ujerumani wamejitokeza mjini Berlin kuwalaki wachezaji wa timu ya taifa walioshinda Kombe la Dunia. Sherehe kubwa zimefanyika katika eneo la Brandenburg Gate, ambapo wacheza… Read More
  • Adebayor augua Malaria,atakosa ziara za Marekani.   Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur Emmanuel Adebayor atakosa ziara ya Marekani baada ya kuukutwa na Malaria. Adebayor, 30, alilazwa hospitali siku ya Jumamosi kwa kile klabu yake imesema "homa ndogo" ya malaria. A… Read More
  • Adidas waingia mkataba mnono na Manchester United.    Kampuni ya Adidas imesaini mkataba wa pauni milioni 750 wa kutengeneza jezi za Manchester United kwa miaka kumi kuanzia msimu ujao. Hatua hii imekuja baada ya mahasimu wao wa Marekani, Nike, kuamua kutoen… Read More

0 comments:

Post a Comment